Friday, March 15, 2013

Mkuu wa wilaya KOROGW E :Changamoto za elimuyetu hapa korogwe

Mkuu wa wilaya KOROGWE, TANGA  ndugu Mrisho Gambo amekutana na haya katika idara ya elimu huko Korogwe baada ya kufanya uchunguzi mdogo wa nini kinaendelea hasa katika matumizi ya pesa, halichokutana nacho ni hiki:
            TAARIFA FUPI


Naendelea kufanyia kazi changamoto za Elimu yetu hapa Korogwe.
Jana nilikutana na Idara za Elimu Sekondari kupitia matumizi ya pesa za kununua vitabu na
vifaa vya kufundishia pamoja na maabara mashuleni.
Nilisema nisianzie mbali sana, nianze toka 2010! Maana bila vitabu na vifaa vya kufundishia hatuwezi kupata Elimu bora.
Jana niliona maajabu na vituko, kwenye baadhi ya shule za sekondari yamekwenda mamilion lakini hakuna vitabu vilivyo nunuliwa. Hata hizo taarifa zilizo andikwa inawezekana zikawa ni za kwenye makaratasi tu na power point.
Ukiuliza unaambiwa mkuu wa shule hapa alipata uchizi, pale alifariki ndo maana hakuna taarifa. Huu ni utani!
Nilihoji Mbona shule hazina maabara lakini pesa za maabara zimetumika? Kwanini Bodi za shule hazishirikishwi? Kwanini walimu hawashirikishwi? Kwanini taarifa za pesa hizi haziendi kwenye mabaraza ya kata? Kwanini taarifa hizi hazitolewi kwenye mikutano mikuu ya vijiji?
Maana hizi ni pesa za umma! Haziitaji usiri wowote.
Sasa nimeamua Mimi na kamati yangu ya Ulinzi na Usalama kupita shule moja baada ya nyingine kukagua vitabu physically.
Tusubiri matokeo, nataka kuwa TOMASO!

Mrisho Gambo

No comments:

Post a Comment

Popular Posts