Wape ng’ombe wako
lishe kamili, yenye nguvu, protini, na vitamin pamoja na maji ya kutosha. Kulisha ng’ombe kwa kutumia aina
yoyote ya malisho haitoshi kukuhakikishia ng’ombe anakuwa na afya nzuri na
kutoa maziwa ya kutosha. Kama ilivyo kwa binadamu, ng’ombe anahitaji mlo
kamili. Malisho ni lazima yawe na uwiano sahihi wa viungo.
Mifugo inahitaji
chakula kitakachowapa nguvu, protini, madini, na vitamin ili kujenga miili yao,
kuzalisha maziwa, na kuzaliana. Wanyama wadogo wanahitaji virutubisho vya
kutosha, ili wakuwe na kuongeza uzito. Ng’ombe wa maziwa wanahitaji virutubisho
zaidi ili kuweza kuzalisha maziwa kwa wingi hasa katika kipindi cha miezi 3-4
ya mwanzo baada ya kuzaa, wakati ambao uzalishaji wa maziwa unakuwa juu.
Malisho ya kijani ni
mlo mkuu kwa mifugo
Mlo muhimu na wenye
virutubisho kwa mifugo ni majani. Lakini soma zaidi
No comments:
Post a Comment