Saturday, September 14, 2013

UTAFITI WA @Twaweza_NiSisi : 83% ya watu hawaikubali kodi ya sh 1,000 kwa mwezi kwa kila laini ya simu #NoSimCardTax

FOR ENGLISH SEE BELOW
 Mnamo tarehe 25 Juni, 2013, bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha wa 2013/2014 ilipitishwa Bungeni.

Siku chache baada ya kupitishwa kwa bajeti, ilionekana kuwa Serikali ilikuwa imeanzisha tozo ya kila mwezi ya TZS 1,000 kwa kila kadi ya simu ya mkononi (Sim card). Jambo la kushangaza lilikuwa, wabunge pamoja na wananchi wa kawaida waliokuwa wakifuatilia hotuba ya bajeti walidai kuwa kodi hiyo, iliyojulikana kama “Kodi ya Kadi ya SIM”, haikujadiliwa Bungeni. Ili lilizua mjadala wa kitaifa miongoni

Sunday, August 25, 2013

MAONI NA MAPENDEKEZO KWENYE KATIBA MPYA ( #BARAZALAKATIKA #ChangeTanzania )


MAONI NA MAPENDEKEZO KWENYE KATIBA MPYA
Ø  UHURU WA KUPATA HABARI.
a)     Uhuru wa jambo hilo la kupata hapbari ni muhimu sana katika sehemu mbalimbali za nchi yetu hii ya Tanzania, hivyo tungependa kupendekeza kuwa ibara ya (30 sehemu ndogo ya 4) ni bora ifutwe katika katiba hii, kwa kuwa kuna kifungu cha 29 (2)b tayari imesha eleza juu ya umuhimu wa namna na haki ya kupata habari kama mwananchi na ni haki yake ya msingi.
b)     Tungependa kuwa ibara ya 30 (4) ni bora iwekwe kwenye sura ambazo zinahusika na usalama wa taifa sura ya 15 kwani inampa fursa na uwanja mpana wa kujadiliwa katika katiba kuliko nafasi ya kujadili ndani ya bunge kwani nafasi ya kujadili ndani ya bunge kwani nafasi yao ni ndogo  na hakuna uwanja mpana kuliko katika katiba.
c)     Kuwepo kwa vyombo vya umma ambavyo havihusiani na vyama vya siasa na view na uhuru

Thursday, August 22, 2013

Taarifa kwa umma wazungumzaji katika Baraza la Katiba la #ChangeTanzania 24/08/2013

Taarifa kuhusu Baraza la Katiba la Change Tanzania (wazungumzaji watakao kuwepo kwenye Baraza )https://www.facebook.com/events/622501621114767/ kama ilivyopangwa Tarehe 24/08/2013, 
Ili kufanikisha kutakuwa na wazungumzaji wafuatao
John Ulanga - Mkurugenzi mtendaji wa Foundation for Civil Society
Dr Azaveli Lwaitama - Mhadhiri wa Chuo kikuu cha Tumaini na mhadhiri mstaafu wa UDSM
Irenei Kiria - Mkurugenzi mtendaji wa SIKIKA
Daniel Welwel - mwanasheria wa Mahakama Kuu, na mwanasheria wa Asyla Attorneys pia mwanaharakati
Deodatus Balile - Mhariri Mtendaji wa gazeti la JAMHURI

From Topics point of view:
Ulanga - Utangulizi – Tanzania tuko wapi na mwelekeo wetu kama taifa?
Dr Lwaitama na Irenei - Uwajibikaji wa taasisi na viongozi kwa wananchi na kuoanisha mfumo wa uwajibishaji
Dan Welwel - Uraia ikiwa ni pamoja na uraia mbili (dual nationality), upatikanaji wa uraia na haki za raia wa Tanzania kwa ujumla
Balile - Uhuru wa kutoa na kupata habari

Friday, August 16, 2013

#ChangeTanzania: Taarifa kwa Umma kuhusu kodi ya laini za simu ( #NoSimCardTax )


‪#‎ChangeTanzania‬ Taarifa kwa umma kuhusu KODI YA LAINI ZA SIMU ( ‪#‎NoSimCardTax‬ ) 

WITO WA WANANCHI KWA BUNGE NA SERIKALI KUHUSU TOZO/ KODI YA LAINI YA SIMU 

Hivi karibuni bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilipitisha muswada wa sheria ya fedha iliyosainiwa na rais Jakaya Kikwete na kuanza kutumika kama sheria kuanzia tarehe 01 August 2013. Sheria hii imetaja chanzo kimojawapo cha mapato kama tozo ya shilingi 1,000 kwa kila laini ya simu (sim card). 
Kama mwitikio wa sheria hii, wananchi wengi kwenye mitandao ya kijamii waliipinga tozo hii na kwa kupitia jukwaa la Change Tanzania, kuanzia tarehe 15 Julai 2013, juhudi zilianza za kukusanya maoni ya wananchi kwa njia mbili: kwa njia ya mtandao – online petition – na kwa njia ya kukusanya sahihi za wananchi mitaani.
Hadi kufikia tarehe 13 August 2013, Change Tanzania kwa njia hizi mbili imekusanya zaidi ya

Monday, July 15, 2013

WITO WA KUSITISHA TOZO/KODI YA LAINI YA SIMU KUFUATIA MABADILIKO YA SHERIA YA KODI 2013


CHANGE TANZANIA timu! Wakati ni kwetu kuonyesha kuwa mabadiliko ni sisi na si kusubiri mtu mwingine alete mabadiliko. Tembelea tovuti hii (http://www.avaaz.org/en/petition/WITO_WA_KUSITISHA_TOZOKODI_YA_LAINI_YA_SIMU_KILA_MWEZI_KUFUATIA_MABADILIKO_YA_SHERIA_YA_KODI_2013/?copy  na uweke sahihi yako kupitia mtandao ili kuikataa kodi au tozo kandamizi ya  laini ya  simu (Sim card tax). Tusaidiane tukusanye sahihi milioni moja ili tuweze kuiwasilisha bungeni mwezi wa nane . Ni dakika chache tu toa muda wako muhimu kulijenga Taifa lako, watanzania tumekuwa na utamaduni wa muda mrefu wa kulalamikia vitu na kuvihacha viendelee japo atukubaliani navyo, kwa kusaini hapo kwenye link kwa pamoja tutakuwa na sauti moja katika ili, pia itasaidia kumtetea mwananchi wa hali ya chini ambaye ndo anaumizwa sana  na kodi au tozo hii kandamizi kila mwezi, serikali inaweza bana matumizi ili kutekeleza bajeti yake, pia kuna vyanzo vingine vya kodi kama tulivyoelezea kwenye hiyo petition. Shawishi na wenzako angalau 100 waweze saini zao pia, kwa kadri tunakavyoweza pata idadi kubwa ndivyo tutakavyopata uwezo wa kusimamisha hii kodi, nchi ni wananchi, sisi ni wananchi.
   Mabadiliko kwa vitendo.

Sunday, June 16, 2013

Maoni ya mdau wa changetanzania juu ya bajeti 2013/2014

1. UTANGULIZI.

Haya ni maoni yangu kuhusu Bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2013/2014. Nimeisoma bajeti yote, hivyo mchango wangu nimeuweka kwenye vipengele vikuu vitatu:

1.) Mipango Mizuri - kwa ajili ya kuwapa motisha viongozi na kuboresha zaidi,

2.) Mipango ya Kurekebisha - ambayo naona ni kandamizi kwa mwananchi, na

3.) Mtazamo wa Jumla na Mapendekezo.

Kwa mambo ambayo nimeona ni ya kawaida sitayagusia; lakini jambo ambalo kwangu ni la kawaida ila kwa wananchi wenzangu linaweza kuwa la mashaka kwao limeligusia.Soma kwa undani hapa changetanzania official website 

Thursday, May 16, 2013

Habari Muhimu kuhusu #Tanzania

1.)  Tanzania: BVR Is for Voter Registration, Not Voting, Says NEC
IN a bid to improve transparency, the National Electoral Commission (NEC) plans to introduce biometric voter registration (BVR) to replace the existing Permanent National Voters Register (PNVR) ahead of the general elections in 2015. Read more 

PRESIDENT Jakaya Kikwete has appointed Ambassador Liberata Mulamula to be Tanzanian Ambassador to the US in Washington.
Prior to the appointment, Ambassador Mulamula was the Senior Diplomacy Advisor to the President. She previously served as the Executive Secretary of the Secretariat of the International Conference of the Great Lake Region (ICGLR) for four years (Januray 2007-December 2010) Read more

3.) Tanzania: 'Cut Down On Tax Exemptions 
AS the Tanzania Revenue Authority (TRA) targets to boost revenue collections to about 18tri/- annually in five years time, Denmark has expressed the need to cut down on tax exemptions to boost revenue collection.
The recent Controller and Auditor General (CAG) report revealed that tax exemptions has reached 1.8tri/-, which is almost 4.6 times of the 8.3tri/-projected to be collected in this financial year Read More

kwa hisani ya  allafrica.com

Friday, March 15, 2013

Mkuu wa wilaya KOROGW E :Changamoto za elimuyetu hapa korogwe

Mkuu wa wilaya KOROGWE, TANGA  ndugu Mrisho Gambo amekutana na haya katika idara ya elimu huko Korogwe baada ya kufanya uchunguzi mdogo wa nini kinaendelea hasa katika matumizi ya pesa, halichokutana nacho ni hiki:
            TAARIFA FUPI


Naendelea kufanyia kazi changamoto za Elimu yetu hapa Korogwe.
Jana nilikutana na Idara za Elimu Sekondari kupitia matumizi ya pesa za kununua vitabu na

MAHITAJI YA NG’OMBE ILI AONGEZE MAZIWA


Wape ng’ombe wako lishe kamili, yenye nguvu, protini, na vitamin pamoja na maji ya kutosha. Kulisha ng’ombe kwa kutumia aina yoyote ya malisho haitoshi kukuhakikishia ng’ombe anakuwa na afya nzuri na kutoa maziwa ya kutosha. Kama ilivyo kwa binadamu, ng’ombe anahitaji mlo kamili. Malisho ni lazima yawe na uwiano sahihi wa viungo.
Mifugo inahitaji chakula kitakachowapa nguvu, protini, madini, na vitamin ili kujenga miili yao, kuzalisha maziwa, na kuzaliana. Wanyama wadogo wanahitaji virutubisho vya kutosha, ili wakuwe na kuongeza uzito. Ng’ombe wa maziwa wanahitaji virutubisho zaidi ili kuweza kuzalisha maziwa kwa wingi hasa katika kipindi cha miezi 3-4 ya mwanzo baada ya kuzaa, wakati ambao uzalishaji wa maziwa unakuwa juu.

Malisho ya kijani ni mlo mkuu kwa mifugo
Mlo muhimu na wenye virutubisho kwa mifugo ni majani. Lakini soma zaidi

Wednesday, March 13, 2013

DEDICATED EFFORTS WILL STOP ACUTE KIDNEY ATTACKS


As kidney disease threaten many life in the world i have honour to share to you a World Kidney Day (WKD), It is a global health awareness campaign focusing on the importance of the kidneys and reducing the frequency and impact of kidney disease and its associated health problems worldwide. The campaign is celebrated every year on the second Thursday of March in more than 100 countries on 6 continents. READ MORE

Tuesday, March 5, 2013

NAFASI YA WALIMU WAPEWE WALIMU NA WATHAMINIWE


Tukubali tukiamini walimu wanajua matatizo yanayoikumba Elimu kuliko mtu mwingine yeyote. Tuwapatie fursa stahiki katika kuleta suluhu matatizo ya Elimu nchini.
Mwalimu ni mlezi wa kiroho, kiakili na kimwili wa wanafunzi. Tatizo la ufaulu mdogo wa wanafunzi wahitimu wa kidato cha 4 mtihani wa mwaka 2012 kwa sehemu kubwa na kwa kiasi kikubwa ni matokeo ya malezi duni, kiroho, kimwili na kiakili ambapo mwalimu amenyang'anywa jukumu lake na kuachiwa kisehemu kidogo tu katika malezi ya kiakili kwa kuwafundisha watoto majibu ya SOMA ZAIDI 

Sunday, March 3, 2013

Maoni ya mwana #ChangeTanzania kuhusu upatikanaji wa raisi ndani ya vyama vya siasa


MAONI BINAFSI YA MABADILIKO YA KATIBA KATIKA KIPENGELE KINACHOHUSU NAMNA YA KUPENDEKEZA NA KUMCHAGUA MGOMBEA WA NAFASI YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KATIKA HATUA ZA AWALI KABISA KATIKA VYAMA VYA SIASA NCHINI:-
(a) Tangu Tanzania imepata uhuru miaka 52 iliyopita ni chama kimoja kimekuwa madarakani katika kipindi chote . Na katika miaka 50 ya uhuru kumetokea kuwa na Marais 4 na wote wametoka chama kimoja tu cha siasa nchini. Historia inaonyesha kwamba katika Marais hao wanne Rais wa awamu ya pili naya tatu walikuwa hawafahamiki kwa watanzania bali kwa vile Rais wa awamu ya kwanza alikuwa ana aminika na watanzania ilibidi watanzania wakubaliane na mapendekezo yake hata kama watanzania hawakuridhika na chaguo la Mwl. Nyerere. SOMA ZAIDI

Saturday, March 2, 2013

Misamaha ya kodi kwa taasisi za kijamii na taasisi za kidini (Charitable Organizations and Religious Organizations)


Suala la misamaha ya kodi limekuwa likizugumzwa kwa muda sasa. Ukweli linawatatiza wengi wetu, wengi tunaweza kuwa hatulifahamu vizuri. Ebu tuangalie sheria inasemaje! Sheria yetu ya kodi inayotumika ni ile ya mwaka 2004 ambayo imefanyiwa marekebisho madogo madogo kadhaa. Kwa sasa naamini toleo linatumika ni lile la mwaka 2006 kwani ndio sheria iliyoko hata kwenye tovuti yaTRA Income Tax Act (Amended), 2006.
Naomba niweke wazi kwamba, kwa mtazamo wangu, sheria yetu iko vizuri kama ikiwa kwenye "mikono salama" nasema mikono salama kutokana na matukio mfano regea kesi ya Bazir Mramba . Lakini mjadala hapa ni misamaha ya kodi.
Katika sheria inayotumika hivi sasa, msamaha wa kodi unaweza kuja kwa namna mbili. SOMA ZAIDI


Maoni Mbadala kwenye ukurasa wa twitter


Wednesday, February 27, 2013

Poor Service is what we hate


Udereva wa namna hii ni hatari kwa maisha yako



TANZANIA TUJIFUNZE KUTOKA NCHI ZINAZOONGOZA KWA ELIMU BORA DUNIANI


Baada ya matokeo mabaya ya kidato cha nne mwaka 2012 nimeshawishika kuandika uchambuzi huu kuhusu elimu na nchi zinazofanya vyema duniani kielimu.
Nchi zinazoongoza kwa elimu bora duniani ni Finland namba moja na Korea ya Kusini inashikilia namba mbili.
Utafiti uliofanyika ili kuzipa hizi nchi mbili nafasi ya kwanza na ya pili ni majumuisho ya matokeo ya mitihani ya READ  MORE

Sunday, February 24, 2013

Barabara ya Mwai Kibaki tunawezaipa jina jipya shiriki mchakato


Kama Change Tanzania tunaungana na wananchi katika masikitiko yao kwa Old Bagamoyo Road kubadilishwa jina na kuitwa Mwai Kibaki Road, maelezo ya wananchi wengi ni kwamba Raisi Mwai Kibaki hana mchango wote katika nchi yetu sasa inakuwaje tunalienzi jina lake (Tuna muenzi Mwai Kibaki) hapa nchini kwa kuweka jina lake katika barabara zetu?.
Change Tanzania kupitia kiongozi wake Maria ilifanya mazungumzo na Meya Jerry Silaa ameeleza Change Tanzania kuwa jina la Kibaki road linaweza kubadilishwa ila haiwezi kuitwa jina lake la zamani Old Bagamoyo Road. Tuko tayari kupeleka maombi na tunahitaji mapendekezo ya jina la barabara. soma zaidi na shiriki hapa  


Saturday, February 23, 2013

Tanzania's headlines 23/02/2013


Dar es Salaam. About a week ago, I read an article in the print media by Prosper Makene titled ‘Arusha institute goes for anti-plagiarism software to promote academic honesty’.
I found it enlightening, as it touched on the negative and positive effects of the internet, particularly in relation to plagiarism at our institutions of higher learning READ MORE

------------------------------------------------------------------------------------------------------------
ZAMBIA has sold 20,000 metric tonnes of maize to Tanzania at a cost of US$7 million. This is under a special bilateral agreement that was facilitated by the countries’ heads of State. An agreement was signed in Lusaka yesterday at the Food Reserve Agency, which will allow Zambia to supply the commodity to Tanzania despite a ban of maize and mealie-meal exports READ MORE

------------------------------------------------------------------------------------------------------------
VENTURES AFRICA – The Tanzania Posts Corporation is to go digital, in line with other posts companies seeking to grow their revenue generation base and to keep pace with technological advancements. Postal office officials and experts told a briefing yesterday that it was READ MORE
------------------------------------------------------------------------------------------------------------
BP Oil, a firm that traded in petroleum business for many years in Tanzania, has expressed interest to invest in natural gas exploration and drilling in the country. READ MORE





Tuimarishe misingi ya uhuru na haki ni muhimu katika maendeleo ya nchi


(a) Kwamba binadamu wote ni sawa;
(b) Kwamba kila mtu anastahili heshima;
(c) Kwamba kila raia ni sehemu ya Taifa na anayo haki ya kushiriki sawa na wengine katika Serikali tangu ya Mitaa, ya Mikoa hadi Serikali Kuu;
(d) Kwamba kila raia anayo haki ya uhuru wa kutoa mawazo yake, ya kwenda anakotaka, uhuru wa kuamini dini anayotaka na wa kukutana na watu mradi havunji Sheria; SOMA ZAIDI

Sunday, February 17, 2013

Tuungane na G20 kupambana na makampuni ya kimataifa ukwepaji kodi

Hii video imechukua mazingira mbalimbali Tanzania/Mtanzania ili kutoa picha halisi ya nchini yetu hasa kiuchumi, hali ya masoko yetu na maliasi tulizo nazo( Tazama hapa ). Kwa maliasili tulizonazo UCHUMI wa wananchi huko chini sana, lazima tujenge mfumo ambao mwananchi ananufaika moja kwa moja na maliasili zilizojaa kila kona, watanzania walio wengi wanaishi maisha duni kama ambavyo hiyo video inaonyesha, wanafanya shughuli za uzalishaji katika mazingira duni, mazingi ambayo hata mteja SOMA ZAIDI

Tanzania yetu katika video, maliasili na shughuli za kiuchumi



ISHI MABADILIKO UYATAKAYO KWA VITENDO (be the change you want to see)

Nilikuwa natafuta sehemu ambayo sitamhukumu Slaa kwa sababu mimi ni CCM, na mwenzangu hatamhukumu kikwete kwa sababu yeye ni CHADEMA bali kutokana na utendaji wao na sera, na ninaposema kuhukumu simaanishi kumwita kikwete fisadi kwenye mtandao, au kuzungumza maisha ya ndoa ya slaa kwenye facebook lakini kumhukumu kwenye sanduku la kura soma zaidi

Shughuli za kiuchumi, #ChangeTanzania #Matukio #Picha


Tuesday, February 12, 2013

MAAMUZI YA KUFUTWA POAC HAYAKUBALIKI TUMWAMBIE SPIKA ANNA MAKINDA NA NAIBU WAKE JOB NDUGAI

Hatua ya spika kufuta POAC imesikitisha sana. Kama Change Tanzania ni muhimu tukashiriki kutetea uwepo wa POAC kutokana na umuhimu wake. Kabla hatujaenda mbali tuweke wazi watu tuliowapa dhamana kuliongoza bunge na mawasiliano yao
Spika Anne Makinda
mawasiliano yake bofya yanapatikana hapa ::  +255 754 465226/+255 784 465226
amakinda@parliament.go.tz  pia unaweza wasiliana naye kwa online form BOFYA HAPA
Naibu spika Ndugai mawasiliano yake bofya yanapatikana hapa
namba zake ni : +255 762 605 951 /+255 655 605 951
 email: jndugai@parliament.go.tz
 Tunaomba wananchi mzungumze na spika na naibu wake kwa njia ya simu hizo hapo juu ili wapete mtazamo mpana kuhusu maamuzi waliyochukua, lakini pia watanzania tuongee nao juu ya utendaji wao kwa ujumla, uvunjwaji wa Kamati ya mahesabu ya mashirika ya umma yaani POAC iwe ni sehemu ya maoni yetu kwao.

Tukiendelea kukaa kimya huku tukilalamika pembeni sio sahihi, yatupasa tuwasiliane nao ili watafakari kwa

Monday, January 28, 2013

Naibu Waziri wa Ujenzi Dr Charles Tibeza na muujiza wa nyumba

Baada ya kuripotiwa wiki iliyopita na moja ya gazeti la IPPMEDIA kwamba naibu waziri wa ujenzi Dr Charles Tibeza anaishi New Africa hotel, waziri huyo sasa amepata nyumba ndani ya wiki moja.
   Hii inaacha maswali mengi ya msingi:
1.) Je waziri alikuwa anaishi hapo hotelini kinyemela? mbona amehama ghafla baada ya kuripotiwa?
2.) Je ni kweli amepata nyumba au amebadisha hotel?
3.) Waziri alikuwa ana kaa hapo kwa bajeti ipi? maana inavyooneka suala lote ni kificho na sababu za yeye kuishi hapo ni siri ya wizara na sasa wanasaka mchawi aliyetoboa hiyo siri.
4.) Walikuwa wanasubiria nini kumhamisha huyo waziri? je ni kweli hakuwa na nyumba ya kuishi? zilikosekana? sasa wamewezaje ndani ya wiki moja?
5.) Mchezo wa serikali kufanya kazi baada ya kulipuliwa utaisha lini?
6.) kwa nini viongozi wetu hasa mawaziri hawatumii nyumba zao kwa makazi? kama hoja ni usalama je kuna

Popular Posts